» » Basi la timu ya B. Dortmund lakabiliwa na milipuko Ujerumani

Basi la timu ya B. Dortmund lakabiliwa na milipuko Ujerumani

Gari la Dortmund lililengwa na milipuko mitatu
Image captionGari la Dortmund lililengwa na milipuko mitatu
Polisi nchini Ujerumani imesema kuwa gari lililokuwa limewabeba wachezaji wa Borussia Dortmund kuelekea katika mchezo wa nyumbani kwenye ligi ya mabingwa Ulaya lililengwa na milipuko mitatu.
Katika mkutano na waandishi wa habari, wamesema kuwa barua ilikutwa pembezoni mwa eneo la shambulizi hilo,lakini haikuwa na maelezo ya kutosha.
Polisi imekana kuwa ni shambulizi la kigaidi.
Mchezaji mmoja wa Dortmund na raia wa Uhispania Marc Bartra amejeruhiwa na kufanyiwa upasuaji.
Mlinzi Marc Bartra amejeruhiwa katika shambulizi hilo
Image captionMlinzi Marc Bartra amejeruhiwa katika shambulizi hilo
Taarifa za kiintelijensia zinasema kuwa zinachunguza shambulizi hilo kama linahusika na mashabiki wa timu ya upinzani.
Mchezo kati ya Dortmund na Monaco umeahirishwa mpaka Jumatano.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440



BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en


tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles