» » USHINDI HATIMAYE- SOMO: MAISHA YA HOFU

USHINDI HATIMAYE- MAISHA YA HOFU
Picha ya Kirumba Seventh-day Adventist Church


Picha ya Kirumba Seventh-day Adventist Church
MHUBIRI: Mchungaji David Mbaga
MAHALI: Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini Mwanza
Mafungu:1 Samwel 27:1-7;Walawi 19:27,28;Rumi 6:3,4;Mathayo 3:16;Mark 16:16
Yesu akamjibu, “Kweli nakuambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu”. (Yohana 3:5)
Watu wamekuwa na hofu na wakaingia katika mambo ambayo mwenyezi (Biblia)Mungu amekataza wakidhani wanatafuta amani pasipo mafanikio.Je ukitumia madawa ya kulevya utaondoa hofu?ulevi,ukahaba,starehe,kunyoa viduku utapata amani?habari gani ukichora mwili wako kwa tattoo ni salama kwako? Maandiko matakatifu yanakataa (Biblia)yanakataa katika (Walawi 19:27,28)
UKIKOSA AMANI HOFU IMETANDA UNAKWENDA WAPI? UNAKIMBILIA KWA WAFILISTI KAMA DAUDI?(1 Samwel 27:1-7)
Yesu Mfalme wa Amani aliye kufa na kufufuka anaondoa hofu zote kwa kila aaminiye na kubatizwa. Kumekuwepo na aina nyingi za Ubatizo ambazo ni kinyume na maagizo ya Mungu kama kunyunyiziwa maji kichwani,kupakwa mafuta,kuruka moto na nyingine nyingi. Ubatizo wa KWELI unapaswa kutanguliwa na Kuamini, Kutubu na kuungama.(Marko 16:16);Mathayo 3:6 inasema “naye AKAWABATIZA katika Mto yordani, huku WAKIZIUNGAMA DHAMBI zao” Matendo.2:38, “TUBUNI MKABATIZWE kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo”
Ubatizo wa kunyunyiza maji kichwani kimsingi haufundishwi katika Biblia bali ni utaratibu ambao umewekwa na wanadamu tu. Kihistoria ulianza mwaka 1311 baada ya mkutano Wa RAVENA,kabla ya hapo wakristo walibatiza ubatizo Wa Biblia Wa watu wazima,na wakuzamisha katika maji mengi..
Katika lugha ya Kiyunani, ambayo ilitumika kuandikia Agano Jipya, kulikuwa na maneno yaliyotumika kwa kunyunyiza na kumwagia. Neno la kunyunyiza ni rhaino, kwa mfano neno hili lilitumika kwa ajili ya kunyunyiza damu. Neno kwa ajili kumwagia ni cheo. Ingawa maneno yote haya yalikuwepo wakati wa kuandikwa kwa Agano Jipya, hayakutumiwa kwa kuhusishwa na ubatizo. Badala yake neno lililotumika katika kwa kuhusishwa na ubatizo ni “baptisma”, ambalo lina mzizi wenye maana zamisha, tumbukiza au tosa.
Biblia inathibitisha kwamba mtu anamwamini kwanza YESU ndio anabatizwa.Kumbe kuwabatiza watoto ni matokeo ya kushindwa kuijua na kuielewa Biblia inavyotaka yenyewe na kufuata mapenzi ya wanadamu. Yohana hakumbatiza mtu ambaye hajatubu, ndio maana aliwahubiria kwanza wakatubu ndipo akawabatiza. Usikimbiekimbie kwa Wafilisti ifuate Biblia,Mungu wa kweli,Mfalme wa amani atakuondolea hofu na utakuwa mtu wa milki yake.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...