Magufuli amteua mkuu mpya wa majeshi Tanzania
Rais John Pombe Magufuli amemteua Luteni Jenerali Venance Mabeyo kuwa mkuu wa majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania akichukua mahala pake jenerali Davis Mwamunyange aliyestaafu.
Taarifa kutoka ikulu iliotumwa katika vyombo vya habari inasema kuwa Luteni huyo sasa amepandishwa cheo na kuwa jenerali kamili.
Mabeyo alikuwa mkuu wa kikosi cha jeshi la nchi kavu kabla ya uteuzi wake.
Wakati huohuo rais amemteua meja jenerali James Mwakibolwa kuwa mnadhimu mkuu wa majeshi ya ulinzi akichukua mahala pake Jenerali Mabeyo.Pia yeye alipandishwa cheo cha luteni jenerali.
Rais amesema kuwa uteuzi huo unaanza kutekelezwa mara moja.
Tarehe ya kuapishwa kwa wawili hao itatangazwa baadaye.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment