» » Yanga yazikimbiza Azam na Simba kwa ubora Afrika

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imewazidi mahasimu wao, Simba na Azam katika orodha ya vilabu bora Afrika na Tanzania kwa mujibu wa orodha iliyotolewa na mtandao wa FootballDatabase.

Kwa mujibu wa orodha hiyo, Yanga inaoongoza ubora Tanzania baada ya kujikusanyia pointi 1252 ikipanda kwa nafasi 14 huku ikimata nafasi ya 332 barani Afrika.


Azam wakisherekea ubingwa wa Mapinduzi

Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Azam wanashika nafasi ya pili nchini Tanzania kwa pointi zao 1249 na kukamata nafasi ya 353 barani Afrika.



Simba wanafunga orodha ya Tanzania katika nafasi ya tatu kwa pointi zao 1247 katika nafasi ya 358 barani Afrika. Hata hivyo Simba ndio timu iliyoimarika zaidi kwa kupanda kwa nafasi 38 toka nafasi waliyokuwa mwaka jana.

Mabingwa wa kihistoria Al Ahly wanaendelea kuongoza barani Afrika wakifuatiwa na Esperance de Tunisia, TP Mazembe, AS Vita na Etoile du sahel wakikamilisha tano bora.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...