» » Waziri wa Nyerere ‘Amchana’ Magufuli


ARCADO Ntagazwa, aliyekuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza, Pili na Tatu amesema kuwa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli, haina nia njema na wananchi wake, anaandika Moses Mseti.

Amesema moja ya kati ya mambo yanayothibitisha kuwa Serikali ya awamu ya tano haina nia njema na wananchi wake, ni msimamo ilionao kuwa Taifa halina njaa.

Ntagazwa ambaye aliwahi kutuhumiwa kuwa si raia wa Tanzania licha ya kuwahi kutumikia wadhifa wa uwaziri katika serikali ya awamu ya kwanza mpaka ya tatu kabla ya kushinda kesi, ametoa kauli hiyo leo alipozungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu.

“Kitendo cha Rais Magufuli kuwauliza wananchi wenya njaa kama wanataka akawapikie, kinasikitisha sana.

“Rais  hawapikii wananchi chakula jikoni, bali anaangalia utaratibu wa kuwatafutia chakula cha msaada katika wakati wa njaa, lakini yeye ameng’ang’ania na kila sehemu anasema hakuna njaa,” amesema Ntagazwa.

Mwanasiasa huyo mkongwe amesema kuwa ametembea katika mikoa ya Simiyu na Mwanza ambapo kuna ukame, hakuna mvua na mazao ya chakula yamekauka sana.

“Wananchi ndiyo ‘mabosi’ na ili uwe kiongozi bora ni lazima uwasikilize watu, lazima ufike sehemu yote ya nchi na uangalie watu wanavyoishi kuliko kuzungumza tu,” amesema.

Kuhusu utumbuaji wa majipu unaoendelea, Ntagazwa amesema mara nyingi Rais Magufuli amekuwa akifanya maamuzi ya kufukuza watu kazi bila kufuata utawala bora, utaratibu na sheria za nchi.

“Utumbuaji majipu si ajabu lakini lazima watumishi waongozwe kwa kufuata utaratibu na sheria za nchi zilizopo, utumbuaji huu si mzuri kwani unasababisha watumishi wengi wa umma wafanye kazi kwa woga badala ya kufuata sheria na taratibu,” amesema Ntagazwa.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...