» » UVCCM Wampongeza Rais Magufuli Kwa Kumtumbua Mkurugenzi Mtendaji TANESCO

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umesema kuwa umefurahishwa na kitendo cha Rais Magufuli cha kupigania maslahi ya wanyonge na kuzuia kupandisha bei ya umeme nchini.

Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka wakati wa kikao cha watumishi wa umoja huo wa kutathmini utendaji kazi wa mwaka 2016 na kuweka utendaji wa mwaka huu.

Shaka amesema kitendo cha Rais Magufuli kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), Mhandisi Felchesm Mramba, ameonyesha uzalendo, ujasiri na upendo kwa wananchi ambao walimpa dhamana ya kuongoza nchi.

“UVCCM tunaunga mkono uamuzi wa Rais wa kuzuia kupanda kwa bei ya umeme na ametazama maslahi ya wananchi waliomchagua kuingia madarakani,”amesema Shaka.

Hata hivyo, amesema kuwa Tanesco kupitia kwa Mkurugenzi wake Mramba aliyetumbuliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo waliwaahidi wananchi kutopandisha bei ya umeme.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...