» » Dk Shein na Maali Seif Watambiana,Shein Adai Hakuna wa Kumng’oa Madarakani hata Yaje Majeshi ya UN ..!!!

seif na shein Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Dk Ali Mohammed Shein na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad jana walihitimisha kampeni za vyama vyao za ubunge wa Dimani ambao uchaguzi wake unafanyika leo kila mmoja akitamba kushinda.
Dk Shein ambaye ni Rais wa Zanzibar, akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Fuoni alirejea kauli yake kwamba hakuna umoja wa mataifa au nchi yoyote inayoweza kumuondosha madarakani.
Dk Shein alisema hayo akiendelea kujibu kauli ya Maalim Seif kwamba siku si nyingi kutatokea mabadiliko makubwa na kwamba wanachama wake wasifadhaike.
Dk Shein alisema CUF walikataa wenyewe kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa marudio uliofanyika Machi 20, 2016, hivyo wanabaki wakitangatanga, “…Wasahau kabisa kuipata nafasi ya urais wa Zanzibar. Hawana uwezo hata wa kuongoza udiwani sembuse urais.”

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...