» »Unlabelled » Watu 12 wauawa shambulio la al-Shabaab Mandera, Kenya

Watu 12 wauawa shambulio la al-Shabaab Mandera, Kenya


Image copyright Ibrahim Adan Ali / Key FM
Image caption Washambuliaji walirusha vilipuzi kwenye jumba hilo
Watu 12 wameuawa baada ya watu wenye silaha kushambulia nyumba moja ya malazi mjini Mandera, kaskazini mashariki mwa Kenya.
Msemaji wa serikali ya Kenya Eric Kiraithe amesema watu sita wameokolewa kutoka kwenye hoteli hiyo ya Bishaaro.
Wanamgambo wanaoaminika kuwa wa kundi la al-Shabaab walishambulia nyumba hiyo mwendo wa saa tisa unusu usiku. Walirusha vilipuzi kwenye nyumba hiyo kabla ya kuingia ndani na kuanza kuwafyatulia risasi waliokuwemo ndani.
"Sehemu ya jumba iliporomoka, na kuua watu 12. Watu sita wametolewa kutoka kwenye vifusi vya jengo hilo wakiwa hai kufikia sasa," ameandika Bw Kiraithe kupitia mtandao wa Twitter.
Wataalamu wa mabomu wanafanya uchunguzi kubaini ni vilipuzi vya aina gani vilitumiwa kutekeleza shambulio hilo.
Image caption Mji wa Mandera unapatikana katika mpaka wa Kenya, Somalia na Ethiopia
Kundi la al-Shabaab limekiri kutekeleza shambulio hilo.
Mji wa Mandera umekuwa ukishambuliwa mara kwa mara na wanamgambo wa al-Shabaab, kundi linalopigana dhidi ya serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa katika taifa jirani la Somalia.
Wanamgambo hao wamekuwa wakishambulia watu ambao si wa asili ya Kisomali.
Image copyright Ibrahim Adan Ali / Key FM
Image caption Maafisa wa usalama nje ya hoteli ya Bishaaro
Asante kwa kutembelea Blog yetu washirikishe na wenzako, Pia tunaomba maoni yako hapa au tupigie kwa (+255) 0769436440 Karibu Tena

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles